Blog hii sasa imehama. Unaweza kutembelea blog hii kupitia Tovuti ya; http://www.gospelnewsmedia.org
Kwa kuitembelea Tovuti hii hivi sasa,Bofya Hapa
Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza.
Blog hii sasa imehama. Unaweza kutembelea blog hii kupitia Tovuti ya; http://www.gospelnewsmedia.org
Kwa kuitembelea Tovuti hii hivi sasa,Bofya Hapa
Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza.
Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Gospel Campaign Centre, la Majumbasita UkongaJijijini Dar es salaam, Moses Magembe, amezindua kampeni maalumu ya maombi na maombezi, kwa muda wa majuma matano, ambapo kazi ya kuwafungua na uponyaji unaoambatana na matendo makuu ya nguvu za Mungu utaanza rasmi.
Akiongea katika Ibada ya hiyo maalum alisema kazi ambayo ameianza haitazimwa bali ameamua kuwasha moto katika siku za Jumatano,Alhamisi,Ijumaa na Jumapili kwa muda wa majuma yote matano fulululizo, hivyo ametoa wito kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam na Vitongoji vyake, wakiwepo watu kutoka mikoa mbalimbali, kujitokeza kwa wingi kuhudhuria maombezi hayo muhimu kwani katika kanisa hilo, masuala ya miujiza siyo kitu cha kushangaza bali watu wamekuwa wakitendewa na Mungu pasipo shaka.
Watu wengi walifunguliwa kupitia Ibada hiyo ya kipekee mara baada ya kuombewa na mpakwa mafuta wa huyo wa Bwana, Mchungaji Moses Magembe ambaye ameamua kujitoa mhanga, kuieleza kweli mbele ya jamii ya Wakristo, na kuipinga imani potofu zilizozagaa nchini, huku akiamua kuendesha Operation maalumu, ya maombezi kupitia jina kuu la BWANA Yesu Kristo.
Mtumishi wa Mungu Nabii na mwimbaji wa nyimbo za injili Faustin Munishi kuzuru GOMA Nchini CONGO DRC leo kwa ziara ya siku tatu ya kiutumishi.
Mtumishi Munishi anatarajiwa kuondoka uwanja wa Jomo Kenyatta airport mida ya saa tatu asubuhi leo na ndege ya Rwanda Air.
Munishi anatarajia Kuhubiri Injili Nchini Congo katika mji wa Goma
sehemu ijulikanayo kama Cadeco Birere. Mkutano huo utaanza tarehe 27 mwezi huu wa 8.
Hapa Munishi anasema “YESU ANAIWEZA GOMA. Atawasamehe wote watakaotubu. Atawaponya wagonjwa wote watakaoamini kwa nguvu yake ya uponyaji. Atayabadilisha Maisha ya wote watakaolikubali Neno lake. Amen”
Nyote Mnakaribishwa
Kilikuwa ni chumba kilichokuwa kimejaa giza sana, jambo nililoweza kuliona kwa haraka ulikuwa ni moto uliokuwa ukiwaka kwa mbali kidogo toka sehemu ile tulipokuwa tumesimama. Bado tulikuwa kwenye chumba kili kile mana ni kirefu sana. Wakanisogeza mpaka karibu na ule moto.
Sikuamini kitu nlichokuwa nakiona mbele ya Macho yangu kwa wakati ule. Machozi yalizidi kunitiririka kwa nilichokuwa nikikiona mbele yangu. Ilikuwa ni sehemu ambayo imetengenezwa kama sehemu ya kuchomea mishikaki hivi, chini kulikuwa na moto mkali sana ukiwaka na juu ya moto kulikuwa na bati flani hivi ambalo liliwekwa vitoto vichanga sana, ambavyo huwa vinatolewa tumboni mwa mama zao angali mama zao ni wajawazito.
Maskini ya Mungu vitoto vile vilikuwa vikichomwa moto na kadri zilivyokuwa vikiyeyuka mafuta yale yalikuwa yakiingia moja kwa moja kwenye bakuli 1 kubwa sana. Mmoja wa waachawi wale wawili alienda moja kwa moja kwenye moja ya bakuli liliokuwa likitumiwa kuhifadhia mafuta yale. Alichukua mafuta kidogo akachanganya na dawa flan zilizokuwa pembeni ya lile bakuli na kuanza kuninyunyizia usoni huku wakiimba wimbo ambao mi sikuweza kuutambua.
Baada ya kama dakika 5 hivi, nikajikuta nimekuwa mtu wa tofauti sana. Gafla nikawa jasiri, mtu nisiyekuwa mwoga. Nilijawa na roho ya unyama kiasi cha kutokuona huruma ya viumbe walw wadogo waliokuwa wakichomwa moto. Kwa wakati huu niliona ni jambo la kawaida sana kwa kitendo kile.
Baada ya wachawi wale kuridhika na hali niliyokuwa nayo kwa sasaiv, walinirudisha kwenye kikao kile na kunikalisha karibu na kiongozi wao. “Sasa unaweza kuzungumza, endelea sasa” Hiyo ndo ilikuwa kauli ya kwanza ya kiongozi yule wa wachawi baada ya mimi kukaa chini.
Kwa wakati huu sikuchukua muda sana kufikiria kwani niliona ni jambo la kawaida tu kula nyama ya mtu. Nilitumia kama sekunde kadhaa hivi na kutoa jibu “Baba yangu”.
NINI KITAENDELEA? JE! NI KWELI BABA YAKE MZAZI EA ESTHER ATAULIWA NA WACHAWI NA KULIWA? NA JE! UJASIRI ALIONAO HIVI SASA ESTHER NI WA MUDA TU AU NI WA KUDUMU?
i. Njia ya kutumia MAWAZO / WAZO
Hii ndio njia kuu ambayo inatumika mara nyingi zaidi. Marko 2:6-8 inasema ”……. Mara (ghafla) Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao…..”. Maana yake ghafla wazo tofauti, na lile alilokuwa akiwaza saa hiyo lililetwa na Roho Mtakatifu ndani yake.
Ukisoma Luka 3:15-16; inasema ”……….Yohana alijibu akawaambia wote,…………”. Yaani alijibu swali ambalo lililetwa ndani yake na Roho Mtakatifu; sio kwamba aliulizwa na mtu yeyote yule.
Luka 20:18-26; inasema ”……….wakamvizia-vizia, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wamnase katika maneno yake, wapate kumtia katika enzi na mamlaka ya liwali. Wakamwuliza wakisema,………………. Lakini yeye alitambua hila yao akawaambia ……………. Wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa”.
Mambo ya kukuwezesha kufanya kazi na njia hii ya mawazo:
a. Jizoeze kukabidhi roho yako, nafsi yako na mwili wako kila siku upya mbele za Mungu.
b. Omba maombi ya vitu vifuatavyo:
SEHEMU YA TANO
Karama ya neno la hekima
I Wakorintho 12:4,8; inasema ” Basi pana tofauti za karama bali Roho ni yeye yule. Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima…….”.
I Wakorintho 14:12 ” ……takeni sana mzidi kuwa nazo ili kulijenga kanisa”.
Karama ya neno la maarifa na neno la hekima zinafanya kazi kwa karibu sana.
Kazi ya karama ya neno la hekima na inavyofanya kazi:
1. kukupa jibu la swali unaloulizwa lakini hasa swali lenye hila, mtego, ushindani au mashtaka ndani yake.
Luka 21:12-15 inasema ”lakini, kabla hayo yote hayajatokea watawakamata na kuwaudhi; watawapeleka mbele ya masinagogi…….. basi kusudieni mioyoni mwenu, kutofikiri-fikiri kwanza, mtakavyojibu, kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga”.
Luka 20:19-26; ”…lakini yeye alitambua hila yao …..”
Marko 3:1-6; inasema ”……….akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza simama katikati ……….nyosha mkono wako. Naye akaunyosha mkono wake ukawa mzima tena”.
Hapa tunaona neno la maarifa (kutambua hila ya wale waliotaka kumkamata) ilianza kufanya kazi, neno la hekima pia likafanya kazi baadaye pale Yesu alipomwambia yule mwenye kupooza ”simama katikati” na tunasoma akaanza kuzungumza na wale watu.
2. inakupa uwezo wa kutatua tatizo lililoko mbele yako.
Mathayo sura ya 1 na ya 2: Habari ya Yusufu na Mariamu. Katika sura hizi karama ya neno la maarifa na la hekima ilifanya kazi kwa kutumia ndoto. Si ndoto zote zinatoka kwa Mungu lakini kama ukiwa na neno la Mungu utatambua ndoto ya Mungu na isiyo ya Mungu.
3. kukupa uhuru wa kushirikiana na watu usiowajua kwa kazi ya Mungu.
Matendo ya mitume 10:1-20; Habari za Petro na Kornelio. Habari hii inaeleza jinsi Petro alivyoona maono wakati amezimia roho (akili zake zilikuwa hazina matunda).
Maono ya aina nyingine, kama tulivyokwishaona hapo nyuma ni ya wazi, ambapo akili zako zinaona na zinaelewa na bado unaweza kuona katika ulimwengu wa roho.
Aina nyingine ni maono ya ndani kwa mfano: unapoomba halafu ghafla ndani yako inakuja picha.
Sasa karama ya neno la maarifa na la hekima itakusaidia kukuwezesha kushirikiana na watu usiowajua.
4. inakurahisishia kuamua kwa haki katika nafasi ya uongozi Mungu aliyokupa au mahali unapohitajika kutoa maamuzi
I Wafalme 3:4-28; habari za mfalme Sulemani, jinsi alivyoomba hekima kwa Mungu na akapewa. Vilevile tunaona jinsi ambavyo aliweza kutoa uamuzi wa haki juu ya kesi ya wanawake wawili waliokuwa wakigombea mtoto. Uamuzi wa haki unahitaji msaada wa Mungu.
SEHEMU YA SITA
Karama ya unabii
I Wakorintho 12:4,10 ”Basi pana tofauti za karama bali Roho ni yeye yule. na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii, na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha.
I Wakorintho 14:12; inasema ”…….takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa”.
Mambo ya msingi kuhusu huduma ya Nabii na karama ya unabii:-
1. kuna tofauti kati ya huduma ya nabii na karama ya unabii.
Efeso 4:11 ”Naye alitoa wengine kuwa Mitume; na wengine kuwa manabii….”. Hapa anazungumza habari ya nabii (ofisi) ya nabii. Huduma ni ofisi na karama ni vitendea kazi katika ofisi.
Kazi za nabii (kama huduma)
Kazi ya karama ya unabii. (kama kitendea kazi):
Ni kujenga, kufariji, kutia moyo na kujirunza, pia huthibitisha kile ambacho Mungu amekwisha kusema na wewe. Katika kitabu cha I Wakorintho 14:3,4,24,25,31; tunasoma ”Bali yeye ahutubuye, asema na watu maneno ya kuwajenga, na kuwafariji, na kuwatia moyo. Yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijenga kanisa. Lakini wote wakihutubu, kisha akaingia mtu asiyeamini, au mjinga, abainishwa na wote, ahukumiwa na wote; siri za moyo wake huwa wazi, na hivyo atamwabudu Mungu, akianguka kifudi-fudi, na kukiri ya kuwa Mungu yu kati yenu bila shaka. Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe”.
2. manabii wapo hata leo ila nafasi zao ni tofauti na za wale wa agano la kale.
Efeso 4:11,14; ”naye alitoa wengine kuwa mitume na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamisisha watakatifu; hata kazi ya huduma itendeke hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa Imani na kumfahamu sana mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu…………. Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja tukizifuata njia za udanganyifu”.
Pia katika kitabu cha Matendo ya Mitume 13:1; tunasoma ”……. Palikuwako manabii na waalimu …..”. hii inaonyesha kuwa manabii wapo hata leo.
Tofauti iko hivi: kwamba manabii hapo zamani (katika agano la kale) walikuwa viongozi wakiongoza watu, yaani walipewa kuongoza watu, lakini katika agano jipya huduma ya nabii ipo ndani ya Kanisa na nabii hakupewa kuongoza kanisa- kila mmoja wakati huu amepewa Roho Mtakatifu ambaye anamwongoza. Hivyo nabii anayesema kwa mausia ya Mungu ni yule anayesema sawasawa na neno la Mungu.
Kanisa linajengwa juu ya misingi miwili ambayo ni:
a. Yesu Kristo
b. Mafundisho ya mitume na manabii ambao wanafundisha mafundisho ya msingi ambayo yanamfanya mtu awe mkristo. (foundation series). Ukisoma kitabu cha Waebrania 6:1; inasema ”kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundishao ya kwanza ya Kristo; tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na Imani kwa Mungu na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu na hukumu ya milele”.
Manabii wa sasa wanatofauti na akina Paulo na akina Petro ambapo hao wa zamani walipewa mafundisho ya msingi na hawa wa sasa wanapewa wito (hekima au special revelation) wanaposoma Biblia wanafungua siri za mafundisho ya msingi, ambayo akina Paulo walifundisha, na kutufunulia sisi.
Yesu alisema katika kitabu cha Mathayo 16:18; ”nitalijenga kanisa langu wala milango ya kuzimu haitaliweza”. Karama zinatokea mahali kama apendavyo Roho. Katika kitabu cha Yohana 14:16, Yesu alizungumza habari za kutuletea msaidizi mwingine, yaani Roho atakapokuja atachukua nafasi ya Yesu katika kulijenga kanisa lake.
Roho Mtakatifu sio karama bali anazo karama, pia Roho Mtakatifu sio nguvu bali anazo nguvu. Tunda la Roho linapofunuliwa ndani ya mtu tabia ya Mungu hujitokeza kwake.
Katika kutafuta vitu vya Mungu, ili kufahamu karama za Roho Mtakatifu na kazi zake, kuna gharama. Mfano, kwenye ndege kuna first class, business class na third class. Ukitaka kupata huduma nzuri zaidi lazima uongeze pesa (gharama) ili upande business class au first class. Lakini dereva wa ndege (captain) ni yule yule. Vivyo hivyo katika maswala ya Mungu wako wanaokaa first, business au third class, lakini wote tunakwenda mbinguni. Hivyo tunahitaji kuingia gharama ili tukae first class ndani ya Yesu. Gharama hizo ni kama:-
i) kusoma neno la Mungu kwa bidii kwa kadri inavyowezekana ili neno hilo likae ndani yako kwa wingi, maan kujua karama za Roho Mtakatifu bila kuwa an maneno ya Mungu ni vigumu.
ii) Maombi n.k.
I Wakorintho 12:1 inasema ‘basi ndugu zangu kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose kufahamu’. Tunahitaji kuwa na hamu ya kuona kwamba karama za Roho Mtakatifu zinafanya kazi na zinafahamika. Hamu hiyo imepotea katika kanisa la Mungu na hivyo kufanya kazi ya ujenzi wa kanisa la Mungu kutofanyika kama Mungu anavyokusudia.
6.) Ujazo wa Roho Mtakatifu. Sio wa siku moja ambao unatosheleza.
Usikose Sehemu ya Muendelezo wa Somo hili Siku ya Kesho.
Inaendelea……………………………………………
Baada ya muda mfupi nilipoteza fahamu zangu kabibsaaaa, na nilikuja kushtuka nikiwa chumbani kwangu. Tofauti na Siku zingine, siku hiyo nilichelewa sana kuamka na niliamka nikiwa mchovu sana. Nakumbuka ilikuwa ni kama mida ya Saa 7 mchana, na hata Bibi hakuniamsha siku hiyo mpaka nilipoamka mwenyewe.
Kabla Sijatoka nje, gafla nikakuta Bibi anaingia Chumbani kwangu. “Esther hujambo?” Alinisalimu Bibi, nikamjibu sijambo na kisha nikamuamkia. Kwakuwa bado nilikuwa na kumbukumbu na tukio zima la jana usiku, nikaanza kumuuliza Bibi, “Kwani Bibi Jana usiku tulikuwa wapi?”. Bibi akasema kwa nini unaniuliza hivyo? Nikamwambia naona mwili wangu umechoka sana na nakumbuka tulitoka hapa usiku tukaelekea sehemu flani hivi ila sikujui ni wapi, na mashavu yananiuma sana.
Kwa kukwepa kunambia ukweli Bibi akaanza kunambia kuwa Niliumwa sana jana usiku na kuzidiwa jambo lililomfanya Bibi kunipeleka kwa mganga. Jibu lake sikulielewa kutokana na mfululizo wa matukio ninaoukumbuka mimi, jambo hili lilinifanya nimuulize Bibi swali lingine, “Kwani Bibi …………” Kabla sijamaliza kumuuliza swali hilo, Bibi akanikatisha, “Wewe nimechoka na maswali yako, hebu nyanyuka uende kuoga, na usimwambie chochote babu yako kuhusu jambo hili, kama akikuuliza kwanini umechelewa kuamka Mwambie ulikuwa hujisikii vizuri, sawa?” Nikamjibu Sawa. Niliamka na kwenda kuoga.
Usiku uliofuata sikupata usingizi kabsaaaaaaa, kutokana na tukio la jana usiku. Na hili lilichangiwa na mimi kulala peke yangu. Niliogopa sana kwakweli na hapa nilishaanza kuamini kwa kiasi flani kwamba Bibi yangu ni Mchawi.
Muda ulizidi kwenda, na katikati ua Usiku nikianza kupata pata usingizi Bibi aliingia Chumbani kwangu kwa kupitia pale pale kwenye ile kona ya Chumba changu akiwa na mavazi kama ya jana usiku. Gafla nilinyanyuka pale kitandani na kujikuta nikianza kulia huku nikimwambia kuwa staki kwenda. Bibi alianza kunibembeleza kuwa leo nitafurahi mwenyewe mana sitapigwa na kuna kitu kizuri wameniandalia.
Sikutaka kumuelewa mambo aliyokuwa akiniambia hivyo nilizidi kulia huku nikiendelea kumwambia kuwa staki kwenda. Majibu yangu yalimpa hasira sana, na kama kawaida yake alichukua madawa yake na kupaka usoni. Pale pale ujasiri uliniisha na nilikuja kushtuka nikiwa kule kule tulipokuwa Jana usiku.
Leo hii kilikuwa ni siku ya Kikao. Kikao ambacho kiliwekwa maalum kwa ajili ya kunikaribisha kwenye kundi lile la Wachawi. Kwa utaratibu waliokuwa wamejiwekea ni kwamba, kila mtu mpya anayejiunga kwenye kundi lile basi ni lazma amtoe kafara ndugu yake 1 wa karibu ili kundi zima la wachawi tumle.
Shughuli ya kumpendekeza mtu huyo huwa ni ya mwenye ndugu hivyo wakanipa nafasi ya Mimi kumtaja ndugu yangu wa karibu ambae nataka wachawi wale wamle. Asikwambie mt, siku ile nilitamani ardhi ipasuke na nitumbukie ndani ili nisiweze kufanya Jambo hilo. Nilianza kuhisi jasho jembamba likinitiririka usoni huku nikiwa natetemeka kwa dhambi wanayotaka niitende.
Je! Nini kitaendelea? Esther atakubali kufanya hivyo? Na kama atakubali, atampendekeza nani? Usikose Muendelezo wa simulizi hii ya kusisimua ili uone ni namna gani nguvu ya Mungu inavyofanya Kazi.